Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

FIFA yaifungia Tabora United kusajili wachezaji

New Content Item (1)
New Content Item (1)

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) imetoa taarifa ya kufungiwa kusajili wachezaji kwa klabu ya Tabora United (Kitayosce) inayoshiriki Ligi Kuu baada ya Evariste Mutambay Kayembe kuhinda kesi ya mdai dhidi ya timu hiyo.

Taarifa hiyo ilieleza kuwa uamuzi huo ulikuja baada mchezaji huyo raia wa Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) alifungua kesi FIFA akidai malipo ya ada ya usajili na malimbikizo ya mishahara

"Uamuzi huo umefanywa na Shirikisho la Kimataifa la Mpira wa Miguu FIFA baada ya mchezaji Evarist Mutambay Kayembe kushinda kesi ya madai dhidi ya kabla hiyo. Mchezaji huyo raia wa DR Congo alifungua kesi FIFA akidai malipo ya ada ya usajili na malimbikizo ya mshahara”

"Klabu hiyo ilitakiwa iwe imemlipa ndani ya siku 45 tangu uamuzi huo ulipotolewa lakini haikutekeleza hukumu hiyo” imesema taarifa hiyo