Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Dewji arudi Simba

Usajili Kassim Dewji afunguka mazito Simba

AWALI kulikuwa na tofauti kati ya Mjumbe wa bodi ya Wakurugenzi Simba, Kassim Dewji na viongozi wengine wa ngazi ya juu kwenye klabu hiyo.

Viongozi wa juu wa Simba walikuwa na maelewano si ya kulizisha na Dewji ambaye alikuwa pembeni ya timu tangu mwezi Desemba mwaka jana.

Baada ya Dewji kuwa nje ya timu kutokana na maelewano yasikuwa ya kulizisha hakufanya jambo lolote kwa timu na aliamua kukaa pembeni na kuangalia tu kinachoondelea kwenye klabu na uongozi.

Mapema mabosi hao wamekutana leo na kufanya kikao kizito kisha kumaliza tofauti zao za hapo awali hadi kushindwa kuwa na maelewano mazuri.

Dewji kabla ya kuondoka kwenye uongozi alikuwa Mwenyekiti wa kamati ya usajili Simba na alisimamia usajili wa dirisha dogo msimu huu.

Baada ya kumaliza kikao hicho na tofauti zao kuisha Mwenyekiti wa bodi ya Wakurugenzi, Salim Abdallah ‘Try Again’ atampangia majukumu kama ni yale yale ya awali au atabaki kwenye uongozi tu.