Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Dar City kuachia kikosi kabla ya Mei 8

Muktasari:

  • Mbwana aliliambia Mwanaspoti, wachezaji wapya na wa zamani walioongezewa mikataba nao watatangazwa siku hiyo.

KOCHA Mkuu wa Dar City, Mohamed Mbwana amesema atatangaza kikosi kitakachoshiriki Ligi ya Kikapu Mkoa wa Dar es Salaam (BDL), kabla ya kufungwa dirisha la usajili Mei 8.

Mbwana aliliambia Mwanaspoti, wachezaji wapya na wa zamani walioongezewa mikataba nao watatangazwa siku hiyo.

Hata hivyo, hakutaka kudokeza majina ya wachezaji wapya na kusisitiza yatatangazwa kabla ya tarehe 8.

“Sisi usajili wetu tunafanya kwa umakini mkubwa, hatumsajiri mchezaji na baadaye  anaondoka,” alisema Mbwana.

Dar City ilifungwa na JKT mwaka jana katika robo fainali kwa michezo 3-1, katika Uwanja wa Donbosco Oysterbay Ratiba iliyotolewa na kamishina wa ufundi na mashindano Haleluya Kavalambi, imeonyesha timu ya Dar City itacheza na Pazi Mei 15.  Huku mchezo wa ufunguzi  Ligi ya mkoa wa Dar es Salaam (BDL) itakuwa Mei 10, ni kati ya bingwa mtetezi wa ligi hiyo JKT na UDSM Outsiders.

Kwa upande wa wanawake DB Liones, bingwa mtetezi,  atacheza na Vijana Quuens, na michezo yote  itachezwa katika Uwanja wa Donbosco Upanga.

Dalili ya Dar City kufanya vizuri katika Ligi ya kikapu ya BDL mwaka huu, ni jinsi walivyoongeza uzoefu zaidi katika mashindano ya kumbukumbu ya mauaji ya Kimbari Rwanda.

Katika mashindano hayo ilifungwa na timu ngumu ya APR kwa pointi 81-68, katika nusu fainali iliyofanyika katika Uwanja wa Petit gymnasium, Rwanda.