Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Azam wafungwa na URA 1-0, Kombe la Mapinduzi

Muktasari:

  • Azam iliyopangwa kundi A pamoja na timu za Simba, Mwenge na Jamhuri za Pemba pamoja na URA ya Uganda waliyocheza nayo leo, itarudi uwanjani kesho Jumamosi kukipiga na Simba  saa 02:15, usiku.

MABINGWA watetezi wa Kombe la Mapinduzi klabu ya Azam FC, imeshindwa kutamba kwenye mashindano hayo yanayoendelea kwenye Uwanja wa Amaan, Kisiwani Zanzibar baada ya kuchapwa bao 1-0 na URA ya Uganda.

URA ilipachika bao hilo dakika ya 32 kupitia kwa Kagaba Nicholas ambaye alipiga shuti kali lililompita tobo mlinda mlango wa Azam, Bedict Haule.

Hata hivyo, licha ya Azam kufanya mabadiliko ya kuwatoa, Yahya Zayd, Masoud na Paul Peter  na nafasi zao kuchukuliwa na  Salim Hoza, Mghana Enock Agyei na Shaaban Chilunda, waliambulia patupu.

Azam ilipata pigo dakika za lala salama baada ya mshambuliaji wao, Enock Agyei kuonyeshwa kadi nyekundu baada ya kurudishia rafu kwa makusudi.

Matajiri hao wa lambalamba wamepangwa kundi A, pamoja na timu za Simba, Mwenge na Jamhuri za Pemba pamoja na URA waliyocheza nayo leo, itarudi uwanjani kesho Jumamosi kukipiga na Simba  saa 02:15, usiku.