Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Aliyempiga kocha Mbeya City afungiwa msimu mmoja

KAMATI ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi ya Bodi ya Ligi Kuu imemfungia kocha wa magolikipa wa Mashujaa FC, Shomari Ndizi msimu mzima wa 2023/24 kushiriki michezo yote iliyo chini ya TFF.

Katika taarifa iliyotolewa na bodi hiyo imeeleza adhabu hiyo imetokana na kosa la kumpiga ngumi usoni kocha mkuu wa Mbeya City, Abdallah Mubiru wakati wa mechi ya mtoano kati ya Mbeya City na Mashujaa iliyopigwa Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya.

Tukio hilo lilitokea wakati Mashujaa wamepata bao na wakaenda kushangilia wakipita benchi la ufundi la Mbeya City ndipo lilipotokea tukio hilo lisilo la kiungwana.

"Amefungiwa kushiriki michezo yote ya Ligi na mashindano yote yaliyo chini ya Shirikisho la Soka (TFF) kwa msimu mzima wa 2023/24 pamoja na kutozwa faini ya Sh2 milioni,"