Kikosi cha Yanga kimeanza safari ya kwenda Tunisia leo kwaajili ya mchezo wa marudiano ya mchujo wa kuwania kucheza hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya wenyeji, Club Africain Novemba 9 jijini Tunis.
Yanga imeondoka na msafara wa watu 41 amabao ni wachezaji 22, benchi la ufundi watu 10 na viongozi wengine watakaombatana na timu.
Mchezo wa kwanza baina ya timu hizo uliochezwa Novemba 2 kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa ulimalizika kwa sare ya bila kufungana, hivyo Yanga inahitaji ushindi wa aina yeyote au droo ya mabao ili kuweza kusonga katika hatua ya makundi.