Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Meneja wa Hermonize azidi kujitanua

ALIYEKUWA meneja  wa msanii Harmonize, Joel Joseph ‘Mr Puaz’  ameanza kujihusisha na baishara ya kuuza nguo za jinsia zote.

Puaz amesema hiyo ni mojawapo ya ujasiriamali na yeye kama mfanyabiashara hawezi akawa anategemea biashara moja.

“Ujasiriamali ni mpana sana  na lazima uwe na vyanzo tofauti tofauti vya kuingiza kipato na zaidi mimi napenda biashara sana sana iwe ni ya bidhaa au ya huduma,” amesema Puaz.

Puaz amesema licha ya kuanza kujihusisha na biashara zingine bado hajaacha kuwameneji wasanii wa muziki.

“Kuhusu suala la kusimamia wasanii hili lipo bado kwenye mchakato wangu na ni moja pia ya biashara zangu, kwa sasa najikita zaidi katika biashara ya bidhaa  na nina matarijio makubwa sana ya kuwa na brandi zangu mwenyewe zikiwemo za nguo, viatu, pochi, mafuta ya kujipaka , miwani na nyinginezo nyingi,” amesema Puaz.