Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Kumbe Paula umaarufu ulimfuata

Muktasari:

  • Paula alisema baada ya kuingia kwenye mtandao wa Instagram kwa kupostiwa na mama yake, watu wakaanza kumshambulia umri wake mdogo na wengine kusema ni mwanafunzi ndiyo umaarufu wake ukakua zaidi.

MTOTO wa mwigizaji Kajala Masanja, Paula amesema katika maisha yake yeye ndiye aliyeutaka umaarufu na umaarufu ukamfuata wenyewe kutokana na kupostiwa na mama yake kwenye mtandao wa Instagram.

Paula alisema baada ya kuingia kwenye mtandao wa Instagram kwa kupostiwa na mama yake, watu wakaanza kumshambulia umri wake mdogo na wengine kusema ni mwanafunzi ndiyo umaarufu wake ukakua zaidi.

"Mimi niliutaka umaarufu na wala watu wasimlaumu mama yangu kwa kumwambia amenilea vibaya, nilikuwa napenda mama akiniposti nafurahi, ila baadhi ya watu walikuwa wanamshambulia mama kwa kuona amenilea katika maadili mabaya, nikawa najiuliza kwani mtu ukipostiwa kwenye mitandao ndio unakuwa na tabia mbaya? Sasa yale mashambulizi yao ndiyo nasema umaarufu ulinifuata baada ya kuwa instagram nikajulikana, lakini baada ya kuwa maarufu nikabadilisha maisha yangu na kutulia katika mahusiamo yangu na kupata mtoto," amesema Paula.

"Kama una nyota ya kujulikana na kuwa staa utajulikana tu, huwezi kuzuiliwa kwa chochote, sababu ya kuwa staa nayo ni kazi, siyo kila mtu anaweza, kuwa nacho hiko ni kapaji, ndiyo maana kuna wengine wanafanya mambo yasiyo na maadili  yakutaka wawe maarufu," ameongeza.