Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Joti ashtukizwa tuzo za HAPAWARDS

Muktasari:

  • Akizungumza na Mwanaspoti, Joti amesema ushindi wa tuzo hauzoeleki ukiwa stejini, hivyo ameruka viunzi vyote na kuweza kupata ushindi wa kuwa mchekeshaji bora wa kiume.

MCHEKESHAJI mahiri nchini, Joti ameshukuru kupata tuzo ya Hollywood And African Prestigious Awards (HAPAWARDS 2024) kwenye kipengele cha  mchekeshaji  bora wa mwaka kupitia filamu yake ya komedi ya 'Maharage ya Mbeya'.

Akizungumza na Mwanaspoti, Joti amesema ushindi wa tuzo hauzoeleki ukiwa stejini, hivyo ameruka viunzi vyote na kuweza kupata ushindi wa kuwa mchekeshaji bora wa kiume.

Joti katika kipengele hicho cha mchekeshaji bora alikuwa anagombania na wachekeshaji wengine ambao ni Masanja Mkandamizaji na Tin White.

Amesema Joti aliposikia ameingia katika ushindani wa tTuzo haikuwa kazi rahisi kwake, kwani  anaujua uwezo wa Masanja na Tin White.

"Namshukuru Mungu kupata hii tuzo, japo ni  za kushtukiza, yaani unapewa taarifa kuwa umeingia katika tuzo bila hata ya kupigiwa kura, tumezoea kupigiwa kura hii ni  unachaguliwa na kupewa taarifa," amesema Joti na kuongeza;

"Komedi yangu ya Maharage  ya Mbeya, ile ya kiboga ndio imenipa ushindi, ushindi ambao hauzoeleki ukiwa stejini, hivyo nimeruka viunzi vyote na kuweza kupata ushindi wa kuwa Mchekeshaji Bora wa Kiume. Tanzania na hizi tuzo zinaandaliwa nje ya nchi basi mimi ni wa dunia."

Hata hivyo, Joti amesema huwa anafurahia komedi zote anazocheza zikiwa za uhusika akiwa amevaa gauni, Babu, Andunje (mtoto mdogo) na zingine nyingi.

Tuzo za  HAPAWARDS zimekuwa zikitolewa kwa miaka saba mfululizo huko Marekani, lakini kwa mwaka huu kwa mara ya kwanza zimefanyika Afrika kwenye ukumbi wa The Super Dome Masaki.