Chaz Baba: Umaarufu samtaim miyeyusho
Muktasari:
- Chaz Baba alieleza kwamba, msanii maarufu anapofanya jambo tofauti jamii humchukulia tofauti hali inayofanya ashindwe ama afikie mafanikio kwa mateso makubwa ya kutafuta kimya kimya.
MTUNZI na mwimbaji mkali wa muziki wa dansi, Chaz Baba amesema umaarufu wakati mwingine ni miyeyusho kwani ugeuka ni mateso kwa kuwa humjengea woga msanii kufanya jambo lolote popote hata kama moyo wake unapenda.
Chaz Baba alieleza kwamba, msanii maarufu anapofanya jambo tofauti jamii humchukulia tofauti hali inayofanya ashindwe ama afikie mafanikio kwa mateso makubwa ya kutafuta kimya kimya.
“Umaarufu kwa msanii ni mzuri lakini ni mateso, uzuri ni kwa kuwa unarahisisha kazi zako lakini ni mateso kwa namna nyingine unatakiwa utende mema tu usikosee kama malaika,” alisema Chaz Baba anayefanya kazi kwa muda mrefu na Twanga Pepeta International.