Mgomo wa Luizio wazaa matunda Simba

Muktasari:

  • "Ijumaa ya juzi, nimejiunga na timu baada ya kusaini mkataba wa mwaka mmoja na sasa naendelea na mazoezi na wenzangu kama kawaida kwani sikugoma kwa makusudi bali nilikuwa nalinda haki yangu," alisema.

Juma Luizio sasa kiroho safi kwani awali aligoma kuambatana na timu ya Simba iliyopo Afrika Kusini, kujiandaa na ligi msimu huu, akidai kupewa mkataba mpya, njia hiyo ilimsaidia kuwafanya viongozi kumuongeza mwaka mmoja.

"Ijumaa ya juzi, nimejiunga na timu baada ya kusaini mkataba wa mwaka mmoja na sasa naendelea na mazoezi na wenzangu kama kawaida kwani sikugoma kwa makusudi bali nilikuwa nalinda haki yangu," alisema.

Ameenda mbali kwamba alijiunga na Simba, kupitia usajili wa dirisha dogo akitokea Zesco ya Zambia, kitu kilichomfanya atumie muda mwingi kuendana na mifumo ya timu ambapo alisema anaamini ligi ijayo atakuwa na wakati mzuri kwani ameanza nao.