Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Hazard bado aiota Chelsea, huku akiri Madrid kiboko

Muktasari:

Hazard alisema licha ya kuishi vizuri akiwa na Chelsea, ameweza kukutana na maisha tofauti akiwa na klabu yake mpya ya Real Madrid.

WINGA mpya wa Real Madrid, Eden Hazard amesema hawezi kusahau maisha aliyoishi akiwa katika kikosi cha Chelsea kwa misimu yote aliyokuwa hapo.

Hazard alisema licha ya kuishi vizuri akiwa na Chelsea, ameweza kukutana na maisha tofauti akiwa na klabu yake mpya ya Real Madrid.

“Tangu nikiwa mtoto nilikuwa naota nitakuja kuvaa jezi ya Madrid, sasa Madrid wakikugongea mlango kitu kilichofuata ni kufungua tu,” alisema.

Aliongeza kuwa mchezaji wa Madrid kumemfanya kutimiza vitu vingi ambavyo alipanga kuvitimiza, lakini pia kufundishwa na kocha ambaye alikuwa anatamani kuwa kama yeye kipindi anacheza.

“Zinedine Zidane ni mmoja ya watu ambao nilikuwa najifunza vingi kutoka kwao kipindi nakuwa, nilikuwa naweka picha zake chumbani kwangu lakini hivi sasa ni kocha wangu.’’