Domayo, Peter waanza matibabu Afrika Kusini

Muktasari:

Hii si mara ya kwanza kwa Klabu ya Azam FC ambao ni mabingwa watetezi watetezi wa Kombe la Kagame kusafirisha wachezaji wao nchini Afrika Kusini kwa matibabu zaidi.

Summary: Azam imewasafirisha wachezaji wao, Frank Domayo ambaye ni kiungo na mshambuliaji Paul Peter kwenda Afrika Kusini kwa ajili ya matibabu zaidi.

Dar es Salaam. Wachezaji wa Azam FC kiungo, Frank Domayo ‘Chumvi’ na mshambuliaji, Paul Peter, walianza matibabu jana Alhamisi nchini Afrika Kusini.

Wachezaji hao ambao waliondoka nchini na Ofisa Mtendaji Mkuu wa Klabu ya Azam FC, Abdulkarim Amin ‘Popat’ siku ya Ijumaa tayari kwa matibabu hayo.

Domayo ambaye pia anaichezea Taifa Stars na Peter akiichezea timu ya taifa ya vijana chini ya miaka 20 'Ngorongoro Heroes'.

Wote wana maumivu ya goti waliyoumia hivi karibuni jambo lililowafanya matajiri wao wa Azam kufanya matibabu ya haraka.

Azam ilishafanya hivyo kwa wachezaji wengine kama, Joseph Kimwaga, Domayo na Pascal Wawa ambaye kwa sasa anakipiga klabu ya Simba.