Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Kipchoge aweka rekodi mpya London Marathon

Muktasari:

Zaidi ya wanariadha 40,000 walishiriki mbio hizo ambazo zimekusanya zaidi ya pauni 1 bilioni

Arusha. Mwanariadha Bingwa wa dunia Mkenya Eliud Kipchoge amezidi kutengeneza rekodi nyingine baada ya kushinda mbio London Marathon akitumia muda was aa 2:02: 38.

Katika mbio hizo Kipchoge ametetea taji lake kwa mara ya nne akitengeneza rekodi mpya baada ya kumaliza wa kwanza akitumia saa 2:02:38, akifuatiwa na Mule Wasihuh aliyemaliza wa pili kwa saa 2:03:16 na nafasi ya tatu ikienda kwa Bashir Abdi 2:07:03.

Kwa upande wa wasichana nafasi zote tatu za juu zimechukuliwa na wanariadha kutoka Kenya wakiongozwa na Brigid Kosgei aliyekata utepe kwa saa 2:18:20, akifuatiwa na Vivia Cheruiyot kwa saa 2:20:14 huku nafasi ya tatu akishikwa na Rosa Dereje aliyemaliza kwa saa 2:20:51