Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Shabiki Senegal afariki akienda uwanjani

SHABIKI Pict

Muktasari:

  • Shirikisho la Soka la Senegal (FSF) lilitoa rambirambi zake juzi jioni, likithibitisha tukio hilo la kusikitisha baada ya Senegal kushinda na kufuzu robo fainali, ikijiandaa kukabiliana na majirani zao wa Mali Ijumaa ya wiki hii.

TANGIER, MOROCCO: SHABIKI mmoja wa Senegal alifariki dunia katika ajali ya gari siku ya Jumamosi akiwa njiani kwenda Tangier ili kuishangilia timu ya Simba wa Teranga katika mechi ya 16 Bora ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2025 dhidi ya Sudan, ambapo wababe hao walipata ushindi wa mabao 3-1 na kutinga robo fainali.

Shirikisho la Soka la Senegal (FSF) lilitoa rambirambi zake juzi jioni, likithibitisha tukio hilo la kusikitisha baada ya Senegal kushinda na kufuzu robo fainali, ikijiandaa kukabiliana na majirani zao wa Mali Ijumaa ya wiki hii.

“Shirikisho la Soka la Senegal limesikitishwa sana kutangaza kifo cha Aïda Faye Samb, kilichotokea kufuatia ajali ya barabarani katika barabara kuu ya Rabat–Kenitra,” FSF ilisema katika taarifa yake. Taarifa iliongeza: “Katika mazingira haya yenye maumivu makubwa, FSF inatoa pole za dhati kwa familia iliyofiwa, wapendwa wake, na familia nzima ya soka.”