Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Messi atakuwepo Kombe la Dunia 2030

Muktasari:

  • Baada ya kiwango chake bora, na huku akiendelea kujenga urithi wake akiwa na jezi ya Albiceleste, wazo jipya limeanza kuzungumziwa: je, Messi anaweza kucheza Kombe la Dunia la saba katika maisha yake, licha ya kuwa na umri wa miaka 42 wakati huo? Nahodha huyo hakuepuka kujibu swali hilo.

DALLAS, Marekani: Timu ya taifa ya Argentina ilianza vyema utetezi wa taji lake la Kombe la Dunia la mwaka 2022 lililoshinda nchini Qatar, baada ya Lionel Messi kufunga mabao matatu (hat-trick) dhidi ya Algeria Jumanne kwenye Uwanja wa Kansas City.

Baada ya kiwango chake bora, na huku akiendelea kujenga urithi wake akiwa na jezi ya Albiceleste, wazo jipya limeanza kuzungumziwa: je, Messi anaweza kucheza Kombe la Dunia la saba katika maisha yake, licha ya kuwa na umri wa miaka 42 wakati huo? Nahodha huyo hakuepuka kujibu swali hilo.

Messi afunguka kuhusu uwezekano wa kucheza Kombe la Dunia la saba 2030, jambo ambalo hadi hivi karibuni lilionekana haliwezekani.

Messi kwanza alitabasamu alipofikiria kuhusu siku zijazo, lakini baadaye alikanusha wazi uwezekano huo.

“Hapana, hapana, kabisa hapana,” alisema Messi. 
“Kama nilivyokuwa nikisema hapa, ukweli ni kwamba tuko katika hali nzuri ya kushindana. Timu hii imeonyesha mara zote kwamba inapambana kwa nguvu na haiwahi kukata tamaa. Haijalishi mpinzani ni nani, daima tunajaribu kutawala mchezo.

“Kipindi cha kwanza hakikuwa rahisi. Inazidi kuwa vigumu kushindana. Tumeona katika Kombe la Dunia kwamba mechi zote zinakuwa na ushindani mkubwa sana, na hakuna anayekupa chochote bure.”

Kwa kauli hiyo, Messi aliweka wazi kwamba mzunguko mwingine wa Kombe la Dunia haupo katika mipango yake kwa sasa, na kwamba lengo lake ni kujaribu kutetea taji la mwaka 2022 katika mashindano yanayofanyika Mexico, Canada na Marekani.

Kufanikiwa kutetea taji hilo ni jambo ambalo limewahi kufanywa na Italia pekee mwaka 1934 na 1938, pamoja na Brazil mwaka 1958 na 1962.

“Tutaendelea kupambana na kutoa kila tulichonacho kwa muda wote tunaoweza,” alihitimisha Messi.

Ingawa ndoto ya kumuona akicheza Kombe la Dunia la saba inaonekana kufungwa na kauli yake mwenyewe, uwezo wake wa kuendelea kuwa muhimu katika kiwango cha juu bado unawashangaza wengi.

Sasa Argentina inajiandaa kucheza dhidi ya Austria tarehe 22 Juni kwenye Uwanja wa Dallas, ikitarajia kuendelea kusonga mbele katika mashindano ambayo huenda yakawa Kombe la Dunia la mwisho kwa Messi akiwa na jezi namba 10.

Argentina itamaliza hatua ya makundi kwa kucheza dhidi ya Jordan tarehe 27 Juni kwenye uwanja huohuo.