Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Mbappe aingia kundi la wababe Madrid

Muktasari:

  • Mshambuliaji huyo wa Ufaransa alifikisha mabao 10 katika kampeni moja ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa mara ya kwanza kabisa katika maisha yake ya soka, wakati Real Madrid ilipoichapa AS Monaco 6-1 katika mchakamchaka wa ligi hiyo usiku wa Jumanne.

MADRID, HISPANIA: SUPASTAA Kylian Mbappe amefanya jambo ambalo ni wachezaji watatu tu katika historia ya Real Madrid waliowahi kulifanya, rekodi safi.

Mshambuliaji huyo wa Ufaransa alifikisha mabao 10 katika kampeni moja ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa mara ya kwanza kabisa katika maisha yake ya soka, wakati Real Madrid ilipoichapa AS Monaco 6-1 katika mchakamchaka wa ligi hiyo usiku wa Jumanne.

Mbappe alifunga bao la kwanza la mchezo huo dhidi ya klabu yake ya zamani baada ya dakika tano tu, akimalizia kwa ustadi kutoka nje kidogo ya eneo la hatari. Bao hilo ndilo lililomwingiza katika klabu ya kipekee, akimfuata gwiji wa soka Cristiano Ronaldo akiwa amevaa jezi ya Real Madrid. Kwa kufikisha mabao 10 katika msimu huu wa Ligi ya Mabingwa Ulaya na kufanya hivyo katika mechi ya sita, Mbappe akawa mchezaji wa nne tu katika historia ya klabu hiyo kufikia idadi hiyo katika kampeni moja. Wengine waliowahi kufanya hivyo ni pamoja na Cristiano Ronaldo (aliyefanikiwa mara saba), Raul na Karim Benzema.

Mbappe aliendelea kuonyesha ubora wake kwa kufunga bao la 11 kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu huu kabla hata ya dakika 30, akimalizia kwa karibu baada ya pasi nzuri ya Vinícius Júnior ndani ya eneo la hatari. Vinícius alikata mpira ndani ya boksi na mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 27 akaongeza bao la pili kwake binafsi. Kabla ya msimu huu, Mbappe hakuwa amewahi kufikisha mabao 10 katika kampeni moja ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, licha ya kukaribia mara kadhaa.

Msimu wa 2020/21, alifunga mabao manane katika mechi 10 akiwa na Paris Saint-Germain na kurudia tena msimu wa 2023/24.

Mshindi huyo wa Kombe la Dunia 2018 pia amewahi kufunga mabao saba katika kampeni moja akiwa PSG, na mara moja alifunga mabao sita AS Monaco alipokuwa kijana. Mabao yake saba kwenye kikosi cha Real Madrid msimu uliopita yalimkaribisha sana rekodi hiyo, lakini sasa hatimaye ameivunja.

Mbappé ni mmoja wa wachezaji wakubwa zaidi katika historia ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, akiwa nafasi ya sita kwa wafungaji bora wa muda wote akiwa na mabao 66. Sasa yuko mbele kwa mabao tisa dhidi ya Thomas Muller na amemkaribia Raúl kwa tofauti ya mabao matano, huku Raúl akiwa na jumla ya mabao 71. Kwa upande wa mabao ya Ligi ya Mabingwa Ulaya akiwa na Real Madrid, Mbappé tayari ana mabao mengi kuliko mastaa wakubwa wa klabu hiyo kama vile Gareth Bale, Luis Figo na Fernando Morientes.