Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Mara paap! Casemiro chama moja na Messi

Muktasari:

  • Nyota huyo wa Brazil ataondoka Manchester United mkataba wake utakapomalizika mwishoni mwa msimu huu.

MIAMI, MAREKANI: KIUNGO wa Kibrazili, Casemiro ameripotiwa kuzivutia klabu za Inter Miami pamoja na timu yake ya utotoni nchini Brazil.

Nyota huyo wa Brazil ataondoka Manchester United mkataba wake utakapomalizika mwishoni mwa msimu huu.

Casemiro, anayefikisha miaka 34 wiki ijayo, alionekana akifurahia mapumziko mafupi ya majira ya baridi mjini Miami pamoja na mkewe Anna wiki hii. Inaeleweka kuwa alikuwa Florida kuchunguza mazingira huku akitathmini chaguo zake baada ya Kombe la Dunia 2026.

Miami ni kati ya klabu kadhaa zinazofikiria kumsajili kiungo huyo wa zamani wa Real Madrid. Klabu hiyo inayomilikiwa na David Beckham imemweka Casemiro juu katika orodha yao ya viungo inaowahitaji baada ya Sergio Busquets kutangaza kustaafu mwaka jana.

Iwapo atahamia klabu hiyo ya Sunshine State, Casemiro ataungana na mpinzani wake wa zamani wa Barcelona, Lionel Messi na kuongeza idadi ya wachezaji waliowahi kucheza na magwiji wawili wa soka, Messi na Cristiano Ronaldo.

Mshindi huyo mara tano wa Ligi ya Mabingwa Ulaya pia amezivutia klabu za FC Porto na Sao Paulo FC, ambako alijiunga akiwa kijana na kuanza taaluma yake ya soka la kulipwa.

Sao Paulo inatarajiwa kumpa Casemiro mkataba wa miaka miwili pamoja na chaguo la kufanya kazi ndani ya klabu baada ya mkataba wake kumalizika. Saudi Arabia pia ni chaguo jingine na kiwango chake cha sasa kinaonyesha bado ana mengi ya kutoa hasa katika michezo yenye kasi ndogo. Anaweza kuungana tena na Cristiano Ronaldo katika kikosi cha Al-Nassr huku Ligi Kuu ya Saudia ikiendelea kuonyesha nia.

Man United imeamua kutokifanyia kazi kipengele cha kuongeza mwaka mmoja katika mkataba wa Casemiro ulioanza mwaka 2022. Klabu hiyo imedhamiria kuepuka mikataba ya muda mfupi ambayo imeleta matatizo hapo awali. Casemiro ni miongoni mwa wachezaji wanaolipwa fedha nyingi katika kikosi cha Man United, akipokea karibu Pauni 350,000 kwa wiki.

Man United inaendelea kwa kasi kuboresha safu ya kiungo, huku Elliot Anderson, Adam Wharton, Carlos Baleba na Alex Scott wakiwa kwenye rada ya wachezaji inaotaka kuwasajili kwenye dirisha lijalo la majira ya kiangazi.


WACHEZAJI WALIOWAHI KUCHEZA PAMOJA NA MESSI NA RONALDO

Angel Di Maria

Sergio Ramos

Gerard Pique

Gonzalo Higuain

Paulo Dybala

Carlos Tevez

Keylor Navas

Deco

Achraf Hakimi

Alejandro Garnacho

Lisandro Martinez

Vitinha

Nuno Mendes

Danilo Pereira

Gabriel Heinze

Miralem Pjanic

Arthur Melo

Andre Gomes

Nelson Semedo

Francisco Trincao

Renato Sanches

Pablo Sarabia

Henrik Larsson

Martin Caceres

Ezequiel Garay

Fernando Gago

Gonzalo Martinez