Kumng’oa Mohamed Salah bonge la ishu

Muktasari:

Inasemekana kwamba Madrid inamfukuzia staa huyo wa kimataifa wa Misri ambaye Liverpool ilimchukua kwa kiasi cha Pauni 37 milioni tu kutoka Roma katika dirisha kubwa lililopita la majira ya joto.

LIVERPOOL imepanga bei ya Pauni 142 milioni kama Real Madrid itaamua kumfukuzia staa wake, Mohamed Salah, katika dirisha kubwa lijalo la majira ya joto.


Inasemekana kwamba Madrid inamfukuzia staa huyo wa kimataifa wa Misri ambaye Liverpool ilimchukua kwa kiasi cha Pauni 37 milioni tu kutoka Roma katika dirisha kubwa lililopita la majira ya joto.