Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Gabriel ajibu tuhuma Arsenal

GABRIEL Pict

Muktasari:

  • Kocha huyo wa Brighton aliikosoa Arsenal katika mkutano wake na waandishi wa habari kabla ya mechi kwa kudai kwamba timu ya Mikel Arteta mara nyingi huchelewesha kuanza tena mchezo wakati wa kona au hata mipira ya kurusha.

LONDON, ENGLAND: BEKI wa kati wa Arsenal, Gabriel Magalhaes amesema hawajali kabisa madai ya kocha wa Brighton, Fabian Hurzeler, kuhusu kupoteza muda makusudi wakati wa mchezo kwenye Ligi Kuu England msimu huu.

Kocha huyo wa Brighton aliikosoa Arsenal katika mkutano wake na waandishi wa habari kabla ya mechi kwa kudai kwamba timu ya Mikel Arteta mara nyingi huchelewesha kuanza tena mchezo wakati wa kona au hata mipira ya kurusha.

Hurzeler, pamoja na wachezaji wake na mashabiki walimlalamikia mwamuzi Chris Kavanagh kuhusu idadi kubwa ya kusimamishwa kwa mchezo wakati Brighton ilipopoteza 1–0 mbele ya Arsenal katikati ya wiki katika Uwanja wa Amex.

Baada ya mechi, kocha huyo wa Kijerumani aliendelea kuikosoa Arsenal akisema kuwa “ni timu moja tu iliyojaribu kucheza mpira wa miguu.” Hata hivyo, beki wa Kibrazili, Gabriel alijibu kauli hizo katika mahojiano mafupi na ESPN Brasil akisema: “Hatuna shida na anachosema. Hilo ni jukumu la mwamuzi kuamua uwanjani. Kama anataka kutoa kadi ya njano au la, yeye ndiye anaamua muda tunaotumia. Sisi tunapaswa kuendelea kufanya mambo kwa njia tuliyozoea na kusonga mbele.”

Arsenal sasa wameongeza pengo hadi pointi saba juu ya msimamo wa ligi, baada ya Manchester City kupoteza nafasi ya ushindi mara mbili na kulazimishwa sare nyumbani dhidi ya Nottingham Forest ambao wanapambana kuepuka kushuka daraja.

Ingawa Gabriel anakubali ushindi huo ni muhimu katika harakati za Arsenal kumaliza ukame wa miaka 22 bila ubingwa, amewataka wachezaji wenzake kubaki makini, aliposema: “Tunapaswa kujikita kwenye sisi wenyewe na kuendelea kama tulivyo. Sasa tumeshinda mechi tatu mfululizo, na lazima tuendelee kushinda. Hilo ndilo jambo muhimu zaidi.”

Baada ya mchezo huo, nyota wa Arsenal, Bukayo Saka pia amesema kuwa timu hiyo haitasikiliza wakosoaji wao katika kipindi cha mwisho cha msimu. Saka amesema baada ya kufunga katika mechi yake ya 300 akiwa na klabu aliyokulia, akisema: “Hatuzisikilizi kabisa hizo kelele. Sizioni wala sizisomi. Hazitusaidii kwa namna yoyote.”