Argentina yajipa matumaini Kombe la Dunia 2026
Muktasari:
- Video zilizosambaa zimemuonyesha Bellingham akishika bega lake la kushoto huku akionekana kuumia baada ya ushindi dhidi ya Norway.
LOS ANGELES, MAREKANI: VYOMBO vya habari nchini Argentina vinaamini nyota wa England, Jude Bellingham, huenda akawa na majeraha kabla ya mchezo wa nusu fainali ya Kombe la Dunia dhidi ya Argentina.
Video zilizosambaa zimemuonyesha Bellingham akishika bega lake la kushoto huku akionekana kuumia baada ya ushindi dhidi ya Norway.
Hata hivyo, taarifa zinaeleza kuwa kiungo huyo amekuwa akisumbuliwa na tatizo hilo tangu alipoumia akiwa Real Madrid mwaka 2025 kabla ya kufanyiwa upasuaji.
Licha ya hali hiyo, Bellingham anatarajiwa kuanza dhidi ya Argentina akiwa tayari amefunga mabao sita katika mashindano hayo.
Baada ya ushindi dhidi ya Norway, Bellingham pia alionekana kutofautiana kimtazamo na kocha Thomas Tuchel kuhusu namna England ilivyocheza, akisisitiza kuwa ushindi ndiyo jambo muhimu zaidi katika hatua hiyo ya mashindano.
Huyu amekuwa mmoja kati ya wachezaji muhimu kwenye kikosi cha England kutokana na kiwangp chake ambacho amekuwa akikionyesha kwenye michezo aliyocheza hadi sasa.
England itaavaana na Argentina kwenye mchezo mkali wa hatua ya nusu fainali leo baada ya jana Ufaransa kuvaana na Hispania kwenye mechi nyingine iliyokuwa na msisimko mkubwa.
Hata hivyo, vyombo vya habari vya England vimesema kuwa mchezaji huyo yupo fiti kwa ajili ya mchezo huo wenye matumaini makubwa kwao.