Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Achraf Hakimi aagizwa kujitokeza mahakamani kwa tuhuma za ubakaji

Muktasari:

  • Tukio hilo liliripotiwa kutokea Februari 2023 katika nyumba yake iliyopo Boulogne-Billancourt. Hakimi anakanusha tuhuma hizo na kudai kuwa alimbusu tu mwanamke huyo, jambo ambalo ameliweka wazi hadharani.

Mlinzi wa Saint-Germain",Achraf Hakimi ameiagizwa kujitokeza mahakamani kutokana na tuhuma za kumnyanyasa mwanamke aliyekutana naye kupitia Instagram.

Tukio hilo liliripotiwa kutokea Februari 2023 katika nyumba yake iliyopo Boulogne-Billancourt. Hakimi anakanusha tuhuma hizo na kudai kuwa alimbusu tu mwanamke huyo, jambo ambalo ameliweka wazi hadharani.

“Nangojea kesi hii kwa utulivu, itakayoonyesha ukweli,” amesema.

Baada ya tuhuma za awali, alipewa uangalizi wa kisheria na kupigwa marufuku kuwasiliana na mlalamikaji. Ikiwa atathibitishwa hatia, anaweza kutumikia hadi miaka 15 gerezani.

Wakili wa Hakimi ameangazia tofauti katika ushahidi wa mlalamikaji, huku wakili wa mlalamikaji akikaribisha uamuzi wa kupeleka kesi mahakamani, akibainisha kuwa unaendana na ushahidi uliokusanywa.

Licha ya kesi hiyo kuendelea, Hakimi amedumu kucheza na PSG na kusaidia klabu kushinda Ligi ya Mabingwa msimu uliopita.

Kesi hiyo itafanyikia katika mahakama ya jinai ya idara nchini France.