Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Zahera ataja Siri ya ushindi Yanga

Muktasari:

MKURUGENZI wa ufundi Yanga, Mwinyi Zahera amesema siri ya ushindi katika kikosi hicho ni morali ya kutosha kwa wachezaji.

MKURUGENZI wa ufundi Yanga, Mwinyi Zahera amesema siri ya ushindi katika kikosi hicho ni morali ya kutosha kwa wachezaji.

Zahera ambaye alikuwa kocha mkuu katika kikosi hicho amerejea tena hivi karibuni na kupewa cheo Cha ukurugenzi wa ufundi.

Akizungumza na Mwanaspoti baada ya ushindi wa 1-0 dhidi ya Simba, Zahera amesema;"Umoja wa viongozi na morali kwa wachezaji ndio Siri ya ushindi."

Zahera amesema wachezaji ndio wanastahili pongezi baada ya kufanya vizuri.

Akizungumzia urejeo wake amesema;"Wananchi wajue mimi ni Zahera mpya."