Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Yanga mbili zote visu

YALAAAH! Kiungo mpya wa Yanga,Geofrey Mwashiuya  akisikilizia maumivu wakati  akichukuliwa vipimo vya afya jana jijini Dar es Salaam. PICHA NA SAID KHAMIS

Muktasari:

  • Kocha wa Yanga, Hans Van Pluijm, alisema kila nafasi katika kikosi chake sasa ina nyota wawili ama watatu wenye uwezo unaokaribiana jambo ambalo linamfanya kuwa na kikosi kipana pengine kuliko timu nyingine yoyote nchini huku Mwenyekiti wa klabu hiyo, Yusuf Manji, akisisitiza kwamba safari hii ameamua kumwaga fedha kusajili na akili yake ipo kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika tu.

UKIIACHA Azam FC kwa klabu zilizofanya usajili mpaka sasa, Yanga ndiyo nyingine inayoweza kutengeneza vikosi viwili imara uwanjani na benchi kukabakiwa na chenji.

Kocha wa Yanga, Hans Van Pluijm, alisema kila nafasi katika kikosi chake sasa ina nyota wawili ama watatu wenye uwezo unaokaribiana jambo ambalo linamfanya kuwa na kikosi kipana pengine kuliko timu nyingine yoyote nchini huku Mwenyekiti wa klabu hiyo, Yusuf Manji, akisisitiza kwamba safari hii ameamua kumwaga fedha kusajili na akili yake ipo kwenye Ligi ya Mabingwa Afrika tu.

Bilionea huyo amesema kwamba anataka kuondoka Yanga kwa kuwaachia kitu cha kujivunia ambacho ni ufanisi kwenye michuano ya kimataifa msimu ujao ambao ni mwakani.

Msimu uliopita Pluijm alilalamika kuwa na kikosi kidogo ambacho kilimpa wakati mgumu katika baadhi ya mechi hasa pale baadhi ya nyota wake walipokuwa majeruhji ama kuwa na ratiba ngumu.

“Nina kikosi kipana sasa, kila nafasi ina wachezaji wawili ama watatu na wote wana viwango vya juu, sina wasiwasi hata pale nitakapokuwa na majeruhi kadhaa kwenye timu. Ushindani mkubwa upo kwa sasa katika timu, kila mmoja anataka kuthibitisha ni bora zaidi ya mwingine, hii inanipunguzia ugumu wa kazi,” alisema kocha huyo wa zamani wa Chelsea ya Ghana.

“Kuna ushindani mkubwa zaidi katika safu ya ushambuliaji, kama unavyofahamu napenda timu yangu ipate matokeo hivyo nafasi hiyo ni nyeti zaidi, wachezaji wa nafasi hizo pia wanakuwa kwenye hatari ya kuumia sana.”

Yanga, mbali ya kuwa na nyota wawili ama zaidi katika nafasi moja, pia ina nyota kadhaa ambao wanamudu kucheza nafasi zaidi ya mbili uwanjani.

 Nyota hao ni Mbuyu Twite anayecheza beki ya kati, pembeni na kiungo, Deus Kaseke, Geofrey Mwashiuya na Simon Msuva wanaomudu kucheza winga zote mbili.

Malimi Busungu pia anamudu kucheza winga na straika wa kati jambo ambalo linampa Pluijm wigo mpana zaidi. Pluijm alisema wiki hii watacheza mechi mbili za kirafiki ambapo leo Jumanne watacheza na KMKM ya Zanzibar na Jumamosi watacheza na kombaini Jeshi ili kukipima kikosi chake.

“Tutacheza mechi mbili za kirafiki, tutacheza na KMKM Jumanne na Jumamosi tutacheza na kombaini ya Jeshi, mechi hizi zitanisaidia kujenga kikosi changu. Natumaini baada ya mechi hizi nitakuwa nimepata picha halisi ya kikosi changu cha kwanza,” alisema Pluijm

ATAJA SIFA ZA FIRST ELEVEN

“Mchezaji wa kikosi changu cha kwanza lazima awe fiti kweli kweli, awe na mawazo chanya na utulivu wa akili, awe pia mpambanaji na kufuata mafundisho yangu ipasavyo. Kikosi kitakuwa kinabadilika kutokana na uwezo wa wachezaji unaoonyeshwa katika mechi na mazoezi ya kila siku, hakuna atakayejihakikishia nafasi,” alisema Pluijm.

VIKOSI VIWILI

Yanga kwa sasa ina vikosi viwili hatari ambavyo havitofautiani sana ubora na Pluijm anaweza kuamua kupeleka kikosi chochote uwanjani na kupata matokeo. Vikosi hivyo ni.

Kikosi cha kwanza

Ally Mustapha ‘Barthez’

James Zuttah

Oscar Joshua

Nadir Haroub

‘Cannavaro’

Kelvin Yondani

Mbuyu Twite

Haruna Niyonzima

Salum Telela

Donald Ngoma

Amissi Tambwe

Simon Msuva

Kikosi cha pili

Deo Munishi

Juma Abdul

Mwinyi Haji

Joseph Mapembe

Pato Ngonyani

Said Makapu

Geofrey Mwashiuya

Andrey Coutinho

Kpah Sherman

Malimi Busungu

Deus Kaseke

Benchi

Benedict Tinocco

Amosi Abel

Edward Charles

Hussein Javu