Wajumbe RT wafukuzwa ukumbini uchaguzi Dodoma

Wajumbe wa Shirikisho la Riadha Tanzania (RT) wametimuliwa ukumbini dakika chache kabla ya kuanza mkutano mkuu na uchaguzi mdogo mjini Dodoma.

Mkutano na uchaguzi huo vilipangwa kufanyika kwenye ukumbi wa Magereza, Msalato.

Ilipofika saa 4:20, wajumbe wakiwa ndani ya ukumbi ilitangazwa oda hawataki kuwaona.

"Hii imetoka kwa mkuu wa jeshi, hamtakiwi kuonekana hapa," alisema mwenyeji na kuondoka bila kutaka maswali.