Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Simba yabadilishiwa uwanja Botswana

Mchezo kati ya Jwaneng Galaxy na Simba wa Ligi ya Mabingwa Afrika hatua ya pili ambao awali ulipangwa kuchezwa kwenye Uwanja wa Taifa wa Botswana, sasa utachezwa kwenye Uwanja wa Obed Itani Chilume mjini Francistown ambao ni kilometa 400 kutoka mji mkuu wa Gaborone.

Mechi hiyo itapigwa Jumamosi Desemba 2 saa 10 jioni, Simba itakuwa ikisaka pointi tatu baada ya kuanza na sare nyumbani huku Jwaneng ikiingia na morali baada ya kuchukua pointi tatu ugenini kwa Wydad Casablanca.

Shirikisho la Soka Afrika (CAF) limetaja sababu ya kufungia uwanja huo ni kutokidhi vigezo huku kikosi cha Simba kikitarajiwa kusafiri Ijumaa.

Meneja Habari na Mawasiliano wa Simba, Ahmed Ally amethibitisha taarifa hizo.