Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Mbosso na Aviola laivu Jangwani 

Muktasari:

  • Yanga imemvuta Mbosso kuwa msanii maalum atakayetumbuiza katika kilele cha paredi la ubingwa wakati timu hiyo itakapomalizia msafara wa kutembeza mataji matano iliyotwaa msimu huu.

Katika makao makuu ya Yanga hapatoshi, baada ya klabu hiyo kumshusha msanii Mbwana Kilungi maarufu kwa jina la Mbosso Khan.

Yanga imemvuta Mbosso kuwa msanii maalum atakayetumbuiza katika kilele cha paredi la ubingwa wakati timu hiyo itakapomalizia msafara wa kutembeza mataji matano iliyotwaa msimu huu.

Yanga imeshatua jijini Dar es Salaam, ikitokea Zanzibar ilipotwaa taji la tano la ubingwa wa Kombe la Shirikisho jana baada ya kuichapa Singida Black Stars kwa mabao 2-0.

Mbosso anayetamba na nyimbo mpya mbili za Power na Aviola atatumbuiza makao makuu ya klabu hiyo  wakati kikosi cha timu hiyo kitakapofika hapo.

Yanga inautumia wimbo wa Aviola kama kijembe kwa watani wao ambao wamekosa mataji msimu huu.

Yanga imechukua ubingwa wa Kombe la Toyota, Ngao ya Jamii, Kombe la Muungano, Ligi Kuu Bara na Kombe la Shirikisho.