Mbao yaikamia Simba

Muktasari:
- Kocha huyo Mrundi alisema Mbao inahitaji ushindi, hivyo hakuna sehemu nyingine ya kuupata tofauti na kwa Simba na mechi nyingine zilizobaki.
Mwanza. Kocha Mkuu wa Mbao FC, Ettiene Ndayiragije amesema wanahitaji kulipa kisasi dhidi ya Simba kwa kuhakikisha wanashinda nyumbani.
Mbao itakuwa mwenyeji wa Simba Aprili 10 mwaka huu kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, Mwanza ikiwa na kumbukumbu ya kuchapwa bao 1-0 katika mchezo wa kwanza uliochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Kocha huyo Mrundi alisema Mbao inahitaji ushindi, hivyo hakuna sehemu nyingine ya kuupata tofauti na kwa Simba na mechi nyingine zilizobaki.
“Mchezo utakuwa mgumu, wenzetu wanataka pointi na sisi tunahitaji, hatuna presha yoyote tumejiandaa kiushindani nahitaji kulipa kisasi kwenye mchezo huu,”alisema Ettiene.
Mrundi huyo alisema amewaandaa vijana wake kisaikolojia na anaamini hawatomuangusha kwenye mchezo huo.