Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Kocha wa Cameroon, Broos akenua pamoja na kipigo cha Chile

Muktasari:

Cameroon 'The Indomitable' ilichakazwa na mabingwa hao wa Amerika Kusini katika mchezo huo wa kwanza wa Kundi B wa mashindano hayo.

Kocha wa Cameroon, Hugo Broos amekisifu kikosi chake kwa kuonyesha soka ya kiwango cha juu dhidi ya Chile pamoja na kupokea kipigo cha mabao 2-0, katika mashindano ya Kombe la Shirikisho la Fifa yanayoendelea Moscow, Russia.

Cameroon 'The Indomitable' ilichakazwa na mabingwa hao wa Amerika Kusini katika mchezo huo wa kwanza wa Kundi B wa mashindano hayo. 

"Nafikiri tulianza mchezo taratibu, tukiwa na hofu kwa sababu tulijua tulikuwa tunacheza na timu bora," alisema Broos.

"Baada ya dakika 20, tulikuwa na uwezo wa kufungwa mabao matatu. Lakini baada ya hapo tulianza kurudi katika mchezo na kipindi cha pili tulicheza vizuri zaidi.

Kocha huyo Mbelgiji anaamini mabingwa hao wa Afrika wamepata cha kujifunza baada ya kipigo hicho kutoka kwa Chile.

"Bao la kwanza la Chile lilipatikana baada ya dakika 80 ni wazi zimetuhudhunisha kwa kuruhusu magoli hayo, lakini tunajivunia namna tulivyocheza kwa kiwango cha juu mchezo huu," alisema kocha huyo.