Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

JK, Manji wafunika mkutano mkuu Yanga

Muktasari:

Katika mkutano huo, kauli mbiu ya wanachama ni mabadiliko ya mfumo wa uendeshaji ambayo Yanga inakwenda kuyafanya.

Rais mstaafu wa Tanzania, Jakaya Kikwete (JK) na Yusuf Manji ndio viongozi walioshangiliwa zaidi na wanachama kwenye mkutano mkuu wa Yanga unaoendelea jijini Dar es Salaam.

Shangwe la mashabiki hao wakati mfadhili na mwenyekiti wa zamani wa klabu hiyo Manji alipoingia ukumbini na wakati Rais mstaafu, Kikwete akiingia lilikuwa mara dufu kulinganisha na walivyowapokea viongozi wengine.

Manji aliingia ukumbini saa 4:58 asubuhi akiwa amezungukwa na makomandoo wa Yanga, kuingia kwake kulisimamisha shughuli ukumbini kwa muda kama ambavyo Rais mstaafu, Kikwete alipoingia ukumbini saa 6:10 na kushangiliwa na wanachama wote ukumbini hapo.

Baada ya Rais mstaafu Kikwete kuingia, wanachama wa Yanga walifungua mkutano kwa sala na duwa kwa dakika 13.