Ikobela ampisha Mwaipasi City ikivaa KMC

Ikobela ampisha Mwaipasi City ikivaa KMC

Muktasari:

  • Mchezo wa raundi ya saba kwa timu ya Mbeya City katika Ligi Kuu ya NBC haijapoteza mechi yoyote na kukaa nafasi ya tatu kwa pointi 10, huku KMC wakiwa nafasi ya 15 kwa alama tano.

Mbeya. Wakati Mbeya City ikishuka dakika chache zijazo uwanjani kuwakabili KMC, Kocha mkuu wa timu hiyo, Mathias Lule amefanya mabadiliko ya mchezaji mmoja, akimpumzisha Winga Frank Ikobela aliyetumika mechi iliyopita dhidi ya Mtibwa Sugar na kumuanzisha Gasper Mwaipasi.

Katika mechi iliyopita Mbeya City ikiwa nyumbani iliizamisha Mtibwa Sugar mabao 3-1 na leo Jumamosi itakuwa Sokoine jijini Mbeya kuwakaribisha KMC mechi itakayopigwa saa 10:00 jioni.

Katika kikosi kilichoanza leo ni Haruon Mandanda, Keneth Kunambi, Mpoki Mwakinyuke, Samson Madeleke, Juma Shemvuni, Aziz Andabwile, Gasper Mwaipasi, Seleman Ibrahim, Paul Nonga, Juma Luizio na Richardson Ng'ondya.

Kwa upande wa KMC, Kocha Mkuu wa timu hiyo, Habibu Kondo amewaanzisha, Farouk Shikhalo, Kelvin Kijiri, Ally Ramadhan, Andrew Vicent Sadalah Lipangile, Abdulrazak Hamza, Abdul Hassan, Kenny Mwambungu, Matheo Simon, Emanuel Mvuyekule, na Miraji Athuman.

Timu hizo zinakutana ikiwa kila upande unakumbuka ushindi katika mechi iliyopita, ambapo KMC waliichakaza Azam FC mabao 2-1 huku Mbeya City wakiishindilia Mtibwa Sugar mabao 3-1.