Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Ihefu yashusha Mnigeria

IHEFU yashusha beki mpya Benjamin Tanimu kutoka Nigeria, baada ya kubadilisha gia juu kwa juu.
Tanimu anakuwa Mnigeria wa pili kuingizwa katika kikosi hicho baada ya kiungo Morice Chukwu kusajiliwa mwanzoni mwa msimu huu akianzia Singida.

Mchezaji huyo, msimu uliopita alijiunga na timu moja Hispania, kabla ya kurejea Nigeria katika klabu yake ya Bendel Insurance.
Beki huyo tayari amewasili kambini kule Arusha akiendelea na mazoezi na wachezaji wenzake na huenda akaonekana uwanjani wakati wowote kuanzia sasa.

Iko hivi. Awali ilikuwa aje mapema kujiunga na Singida Fountain Gate, lakini baadaye akahamishiwa Ihefu, akiwa ni miongoni mwa wachezaji wakigeni waliopelekwa katika kikosi hicho kipya.
Wachezaji waliohamishwa kutoa Singida kwenda Ihefu ni pamoja na Morice Chukwu, Marouf Tchakei, Joash Onyango, Mukrim Issa, Elvis Rupia,Khomeiny Khomeiny.

Ihefu imeshacheza mechi tatu za kirafiki mbili dhidi ya Mbuni na wameshinda zote, kisha kutoka sare mbili dhidi ya TMA na Polisi Tanzania.

Kwa sasa timu hiyo ipo jijini Arusha ikiweka kambi kabla ya kumalizia mechi ya kiporo cha duru la kwanza la Ligi Kuu Bara inayorejea leo kwa pambano la Kagera Sugar dhidi ya Yanga, kisha kuanza kujipanga kwa mechi za duru la pili la ligi hiyo inayoongozwa kwa sasa na Azam FC yenye pointi 31.