Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Amir Maftah aeleza alivyotaabika kucheza soka Msumbiji

Muktasari:

Maftah aliachwa Yanga mwaka 2010 na kutimkia kwa watani zao wa jadi Simba kabla ya kwenda Msumbiji

Dar es Salaam.Beki wa zamani wa Yanga, Simba na Kagera Sugar, Amir Maftah amesema alipata wakati mgumu kuzoea maisha ya soka ya Msumbiji.

Maftah anayechezea klabu ya 3 de Fevereiro de Quelimane ya Ligi daraja la kwanza au Segunda amesema uvumilivu ndiyo umemsaidia.

Maftah sasa ametimiza miaka miwili akicheza soka la kulipwa Msumbiji amesema licha ya kupewa ushirikiano na wenyeji, lugha ya Kireno ilimsumbua.

"Nilipata tabu mno kuzoea mazingira, lugha na asili ya huku, lakini nilivumilia na polepole nimeanza kuzoea," alisema mchezaji huyo.

Alisema Msumbiji wana tamaduni za kizungu zaidi kulinganisha na Tanzania ambako aliishi na kuzoea miiko na tamaduni za kiafrika.