Ajib ajisalimisha Yanga
Muktasari:
Mshambuliaji huyo alikuwa na mchango mkubwa Yanga msimu uliopita
Morogoro. Hatimaye mshambuliaji Ibrahim Ajib amewasili kambini Yanga Mkoani Morogoro.
Ajib ametua mazoezini asubuhi hii akiwa pamoja na wenzake.
Ajib alionekana kukimbia peke yake nje ya uwanja baada kukosa sehemu kubwa ya mazoezi na wenzake.
Kuwasili kwa Ajib kunafanya sasa kusalia mchezaji mmoja pekee Mohammed Issa 'Banka' ambaye bado hajajiunga na timu hiyo.