Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Mugalu: Napitia kipindi kigumu

Mugalu: Napitia kipindi kigumu

CHRIS Mugalu alimaliza msimu uliopita na mabao 15 akishika nafasi ya pili ya wafungaji bora nyuma ya John Bocco, lakini msimu huu straika huyo mambo yamekuwa magumu kwake na kukiri kuwa anapitia kipindi kigumu.

Mugalu alisema katika maisha yake ya soka la ushindani hajawahi kupitia kipindi kigumu kama wakati huu ndani ya Simba.

“Kuna wakati huwa nashindwa kufunga, ila haijawahi kuwa kipindi kirefu kama hiki nilichonacho Simba, kwani mara nyingi hata nikitoka majeruhi nikirudi naendelea na ukali wangu wa kufunga mabao,” alisema Mugalu.

Straika huyo alisema kwa sasa analichukulia changamoto anayopotia kama darasa la kujifua zaidi ili arejeshe makali yake binafsi kwa faida ya timu ya Simba.

“Binafsi naimani kubwa mno huu ni mwisho kwangu kucheza mechi nyingi bila kufunga nimefanya mazoezi yangu binafsi pamoja na kujiandaa vya kutosha kusikiliza yale ya benchi la ufundi ili kwenda kutimiza yale ambayo kila mmoja anatamani kuona kutoka kwangu,” alisema mchezaji huyo.