Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Kifo cha Sonso chaitesa Ruvu

RIPOTI MAALUMU: Mapya kifo cha Sonso

KOCHA Mkuu wa Ruvu Shooting, Boniface Mkwasa ‘Master’ amesema msiba wa beki wao, Ally Mtoni ‘Sonso’ bado unawatesa nyota wa kikosi cha timu hiyo na kama kocha ameamua kukomalia kuwajenga kisaikolojia ili wakae sawa.

Nyota huyo wa zamani wa kimataifa wa Tanzania, alisema licha ya ushindi wa bao 1-0, dhidi ya Tanzania Prisons bado amewaona wachezaji wake hawako vizuri kutokana na kuondokewa na mchezaji mwenzao.

“Itawachukua muda kidogo kurudi katika hali yao ya kawaida ukizingatia hata mchezaji aliyekuwa akilala naye chumba kimoja bado hajawa sawa kisaikolojia, hivyo naendelea kuwajenga li kurejea kwenye hali zao za kawaida,” alisema Mkwasa na kuongeza;

“Tunaendelea na maandalizi ya michezo yetu inayofuata, kama unavyojua hatupo katika nafasi nzuri katika msimamo wa ligi, hivyo tunahitaji kupambana ili tuweze kujinasua kwenye nafasi za chini.”

Sonso aliyewahi kuzichezea Lipuli, Yanga, Kagera Sugar na pia timu ya taifa, Taifa Stars alifariki dunia Februari 11, 2022, katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili kutokana na matatizo ya mguu.

Ruvu kwa sasa ipo nafasi ya 13 ikiwa na pointi 15 baada ya kushuka uwanjani katika mechi 15, ikishinda nne, sare tatu na kupoteza nane.