Kibu kuwamaliza mabosi wake

Kibu kuwamaliza mabosi wake

Muktasari:

  • Kibu kabla ya kutua Msimbazi alikiwasha Mbeya City na leo kwa mara ya kwanza atakutana nao katika vita ya kusaka alama tatu.

Mbeya. Straika Kibu Denis kwa mara ya kwanza leo atakutana na waliokuwa mabosi wake wa zamani baada ya kupewa nafasi ya kuongoza eneo la ushambuliaji kuimaliza Mbeya City katika mchezo wa Ligi Kuu utakaopigwa hapo baadaye.

Denis ambaye aliitumikia Mbeya City msimu uliopita, leo pamoja na nyota wengine atakuwa na shughuli pevu kuthibitisha ubora wake kuhakikisha anaisaidia timu hiyo kuondoka na alama tatu.

Kikosi kilichowekwa hadharani cha Wekundu chini ya Kocha wake, Pablo Franco ni pamoja na Aish Manula, Shomari Kapombe, Henock Inonga, Joash Onyango, Mohamed Hussein, Mzamiru Yassin, Jonas Mkude, Sadio Kanoute, Benard Morrison, Chris Mugalu na Kibu Denis.

Benchi wapo Beno Kakolanya, Israel Naenda, Paschal Wawa,Pape Sakho, Maddie Kagere, Jimmyson Mwanuke, John Bocco, Hassan Dilunga na Kennedy Juma.