Klabu ya Manchester United imethibitisha kujenga uwanja mpya wenye uwezo wa kuingiza mashabiki 100,000 karibu na uwanja wa sasa wa Old Trafford.
Taarifa ta ujenzi wa Uwanja huo mpya imekamilisha mpango kazi wa mmiliki mwenza wa Man United Sir Jim Ratcliffe, ambaye aliahidi kufanya hivyo kufuatia uchakavu wa Uwanja wa Old Trafford.
Gharama za ujenzi wa Uwanja mpya zinatajwa kufikia Pauni2 bilioni.