Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Kusah afichua ndoto ya kumuoa Ruby

KUSAH

Muktasari:

  • Kusah ambaye amepata mtoto mmoja na Ruby ndoto yake ya kumuoa ilizimika na aliwahi kusema watafunga ndoa, kabla ya kuachana na kwa sasa yupo kwenye penzi la Aunty Ezekiel.

Msanii wa Bongo Fleva, Kusah amesema kuzaa na mwanamke haina maana ni lazima amuoe, baada ya kuulizwa endapo alikuwa na mipango ya kumuoa mpenzi wake wa zamani, Ruby kabla ya kuachana.

Kusah ambaye amepata mtoto mmoja na Ruby ndoto yake ya kumuoa ilizimika na aliwahi kusema watafunga ndoa, kabla ya kuachana na kwa sasa yupo kwenye penzi la Aunty Ezekiel.

KUS 01

"Siwezi kusema hatukuwa tumeendana na Ruby ndiyo maana sikumuoa, hapana, ila siyo lazima ukizaa na mwanamke ndiyo uje umuoe. Hata kama niliwahi kusema tutafunga naye ndoa, yawezekana mipango iliharibika kabla ya kufikia lengo hilo hivyo tukabaki kuwa wazazi ambao tunaheshimiana na uzuri kila mmoja ana mahusiano yake mengine kwa sasa. Ndiyo maana nimesema mnaweza tu mkazaa na mwishowe kila mtu akaendelea na mambo yake na hiyo desturi siyo ya kwangu peke yangu ipo dunia nzima."

KUS 02

Kusah ambaye pia ni mwandishi wa nyimbo na ndiye aliyemwandikia pia Ruby wimbo wa Ntande na Alele, amewahi kutamba na nyimbo kama I wish, Nilewe, Nakupenda, I don't Care, Hujanikomoa na nyingine nyingi.

Hivi karibuni alizindua EP yake 'Bumbuli Boy' ikimaanisha nyumbani kwao Bumbuli mkoani Tanga. Pia amefichua ameshamuoa Aunty kimya kimya  muda mrefu.