Kifo cha Ashly Robinson Zanzibar chazua maswali, familia yataka ukweli
Muktasari:
- Ashly alifariki wakati akiwa mapumziko Zanzibar pamoja na mchumba wake, Joe McCann, ambapo alikuwa akisherehekea siku yake ya kuzaliwa pamoja na uchumba wake tukio lililotarajiwa kuwa la furaha kabla ya kugeuka kuwa msiba.
Wazazi wa Ashly Robinson, ambaye alikuwa mshawishi wa mitindo ya maisha kutoka Marekani aliyefariki dunia akiwa na umri wa miaka 31 katika mazingira yanayotajwa kuwa na utata visiwani Zanzibar, wamezungumza kwa mara ya kwanza na vyombo vya habari wakielezea majonzi yao na kutaka ukweli ujulikane kuhusu kifo cha binti yao.
Ashly alifariki wakati akiwa mapumziko Zanzibar pamoja na mchumba wake, Joe McCann, ambapo alikuwa akisherehekea siku yake ya kuzaliwa pamoja na uchumba wake tukio lililotarajiwa kuwa la furaha kabla ya kugeuka kuwa msiba.
Kwa mujibu wa wazazi hao, waliwasiliana kwa mara ya kwanza na mchumba wa Ashly takribani saa 11 baada ya tukio linalodaiwa kusababisha kifo chake. Baadaye, walipokea taarifa rasmi kutoka hoteli aliyokuwa amefikia kwamba binti yao alikuwa amefariki dunia.
Familia hiyo imesisitiza kuwa inaendelea kutafuta majibu kuhusu mazingira halisi ya kifo hicho, huku maswali mengi yakibaki bila majibu.
Wakati huohuo, CBS News imesema imejaribu kuwasiliana na kampuni ya mchumba wake, Asymmetric, kuomba maelezo, lakini hakukuwa na majibu yaliyotolewa. Aidha, Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani imethibitisha kifo cha raia wake mmoja huko Zanzibar, lakini haikutoa taarifa zaidi ikieleza sababu za faragha.
Taarifa iliyotolewa jana na Polisi Mkoa wa Kaskazini Unguja, Zanzibar wamedai kuwa kifo cha Robinson (31) kimetokana na kujinyonga katika chumba cha hoteli. andaa kichw cha habari maneno tisa