Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Chino ahamishiwa Muhimbili, dereva afariki


Mtu mmoja aliyetambulika kwa jina la Nabeel ambaye alikuwa dereva kwenye gari lililombeba mwanamuziki na mnenguaji, Isaya Mtambo maarufu ‘Chino Kid’ pamoja na wenzake, amefariki dunia kufuatia ajali ya gari iliyotokea siku ya jana.

Asubuhi ya leo Mtayarishaji wa muziki ‘Abbah Process’ amethibitisha taarifa hiyo ya masikitiko ambapo amesema wamempoteza mwanafamilia mwenzao ambaye amemtaja kwa jina la Nabeel.

Hata hivyo inadaiwa kuwa Chino amepata majeraha sehemu ya kifua na sasa yupo Hospitali ya Taifa Muhimbili huku baadhi ya ‘madansa’ wake wakidaiwa kuvunjika miguu.

Ajali hiyo ilitokea jana Jumamosi Novemba 11, 2023 eneo la Kabuku mkoani Tanga ambapo gari lao aina ya Toyota Alphard liligongana na lori la mafuta.