Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Gabo: Wasanii wenzangu wananionea wivu

MSANII wa Filamu nchini, Salim Ahmed 'Gabo'

Muktasari:

  • Gabo ni miongoni mwa wasanii wa filamu wanaofanya vizuri huku akiwa na rekodi ya kushinda tuzo mbalimbali.

MSANII wa Filamu nchini, Salim Ahmed 'Gabo' amesema wasanii wenzake wamekuwa wakimuonea wivu.
Gabo ambaye ameteuliwa kuwa balozi wa kampuni ya simu ya Tecno amesema tangu amepata nafasi hiyo amejitofautisha na wasanii wengine.
Msanii huyo alibainisha hayo wakati wa uzinduzi wa simu ya Tecno Phantom 9 ambayo imeanza kuuzwa kwa oda maalumu nchini.
"Kabla ya uzinduzi huu, mabosi wangu walileta simu za Phantom 9 tatu pekee nchini, ambayo moja ni ya hii ya kwangu," alisema Gabo na kuendelea.
"Kwa huduma ambazo ziko kwenye hii simu, wasanii wenzangu kila nilipokwenda walinionea wivu, lakini bahati mbaya hawakuwa na uwezo wa kuipata hivyo kwani hazikuwepo nchini," alisema.
Alisema alijitofautisha nao ingawa sasa Tecno imeamua kuleta Phantom 9 kwa oda maalumu.
Meneja uhusiano wa Tecno, Eric Mkomoye amesema Gabo amekuwa balozi wao wa tofauti na kusisitiza kuwa ujio wa Phantom 9 utarahisha mambo mbalimbali kwa watumiaji ikiwamo wasanii.