Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Ben Paul: Bado nipo kwenye gemu

Muktasari:

Ben Paul ameibuka na kibao cha sikukuu ya Krimasi alichokiita ni zawadi kwa ajili ya mashabiki wake na kuwasisitiza kwamba yupo ndani ya gemu na wataendelea kufurahia burudani yake.

MSANII wa Bongo Fleva, Benard Paul 'Ben Paul' amekuja na kibao kinachoitwa Sikukuu baada ya ukimya wa muda mrefu, alichosema ni maalumu kwa ajili ya mashabiki wake.

Ben Paul amesema ameamua kuwatakia kheri mashabiki wake kupitia kibao hicho, akiamini watafurahia kusikiliza burudani hiyo.

Ben Paul amesisitiza kwamba bado anazifanya kazi za muziki tofauti na watu wanavyomuona amepotea kwenye gemu.

"Nimeona nifanye uungwana wakuwapa zawadi ya wimbo mashabiki wangu ili waweze kufurahia sikukuu za Krimasi na kuvuka salama mwaka mpya,"

"Kuna mashairi nilioimba kwamba wapo wenzetu ambao wametangulia mbele ya haki sisi ni nani kwa Mungu tunapaswa kushukuru, hakika ni nyimbo nzuri naamini wataifurahia," amesema.