Mastaa Simba wafundwa

Muktasari:

"Sina wasiwasi na uwezo wao ila wanatakiwa kuwa watulivu, waepuke papara, mipira ya shoo badala yake wafanye kazi yenye madhara ya kuifanya timu iweze kuwa na taswira ya ubingwa," alisema.

BEKI wa zamani wa Simba, Frank Kasanga 'Bwalya' ameshauri nyota wa kikosi hicho kwamba wapo vizuri kiuwezo, ila wanatakiwa kuwa watulivu na kujiamini kile wanachokifanya uwanjani kwa madai watafika mbali.

"Sina wasiwasi na uwezo wao ila wanatakiwa kuwa watulivu, waepuke papara, mipira ya shoo badala yake wafanye kazi yenye madhara ya kuifanya timu iweze kuwa na taswira ya ubingwa," alisema.

Amewaambia wachezaji wa timu hiyo,kwamba wakifanikiwa kutwaa ubingwa msimu huu, watakuwa wamejiandakia rekodi ya kutopata taji hilo ndani ya miaka minne.

"Mchezaji mwenye mtazamo wa kufika mbali ni yule anayehitaji kuweka alama kwa kila timu atakayoitumikia lakini kwa wale ili mladi liende hawaoni hasara juu ya hilo, watwae ubingwa sawa wakikosa sawa," alisema.

Staa huyo anasema ni wakati wa wachezaji kulipa fadhira na kuelewa kwamba wamesajiliwa kwa kazi maalumu akisisitiza kuwa  kamati ya usajili ilitumia  gharama tofauti na misimu iliyopita ili kifanyike kitu tofauti na ligi zilizopita.

"Vitu vingine vya kujiongeza wenyewe kama ni gharama za usajili vyombo vya habari vimeweka wazi, hilo tu wanapaswa kulielewa kwamba ubingwa unahitajika na siyo wao wajae upepo kujiona wapo juu ya malengo ya klabu," alisema.