VIDEO: Haji Manara amuibukia Ibrahim Ajib

Msikie msemaji wa klabu ya Simba, Haji Manara anavyosema, eti katika wachezaji wote wa klabu ya  Yanga akiambiwa ni yupi amchukue amesema ni mshambuliaji  wao Ibrahim Ajib.

Haji ambaye kwa kawaida huwa haishiwi vituko kutokana na maneno yake ya utani, amejibu swali hilo baada ya kuulizwa na mchambuzi wa soka na mwandishi  wa gazeti la Mwanaspoti, Edo Kumwembe.

"Kati ya wachezaji wote Yanga, Ajibu namrudisha,"alijibu Manara tena kwa kujiamini.

Ajibu mchezaji wa zamani wa Simba aliyoichezea kwa misimu mitatu, lakini mwanzoni mwa msimu huu, alisajiliwa na Yanga anayoichezea mpaka sasa.