Azam waichapa Jamhuri mabao 4-0
MABINGWA watetezi wa Kombe la Mapinduzi klabu ya Azam FC, imeendeleza ubabe katika
michuano hiyo baada ya kuifunga Jamhuri ya Pemba mabao 4-0, katika mchezo uliopigwa Uwanja wa
Amaan, Zanzibar.
Azam walifunga mabao yao dakika ya 16 kupitia kwa straika Mghana Bernald Arthur aliyepokea
krosi ya Bruce Kangwa.
Kipindi cha pili kilipoanza dakika ya pili, Salmin Hoza aliifungia Azam bao la pili kwa shuti lililokwenda
moja kwa moja nyavuni, pasi ikitoka kwa Yahya Zaiid.
Zaiid naye aliibuka na kufunga bao la tatu dakika ya 54 kutokana na mpira wa adhabu na wakamaliza kalamu ya mabao yao dakika 79 kupitia kwa Paul Peter .
Hata hivyo, Jamhuri walipata pigo kipindi cha kwanza dakika ya 43 baada ya beki wao, Abdul
Mahafudh kuonyeshwa kadi nyekundu kwa kumchezea vibaya kiungo wa Azam Joseph Mahundi,
Huo ni mchezo wa pili wa Azam katika mashindano hayo ambapo mchezo wa kwanza, waliifunga
Mwenge ya Pemba mabao 2-0.