Mabao ya Obrey Chirwa yawashtua mashabiki Yanga

Muktasari:

Chirwa sasa amefikisha mabao 10 akiachwa magoli mawili na Emmanuel Okwi anayeongoza akiwa na mabao 12 huku akimpita John Bocco mwenye mabao 9.

Dar es Salaam.  Mshambuliaji wa Yanga, Obrey Chirwa amefunga mabao mawili katika  dakika ya 46', 65 na 87 huku la Emmanuel Martin dakika ya 69.
Chirwa sasa amefikisha mabao 10 akiachwa magoli mawili na Emmanuel Okwi anayeongoza akiwa na mabao 12 huku akimpita John Bocco mwenye mabao 9.
Ushindi wa Yanga utaisaidia kupunguza uwiano wa pointi dhidi ya wapinzani wao Simba waliopo kileleni na pointi 38.
Chilwa amekuwa akitazamwa  na mashabiki wa klabu hiyo hasa katika idara ya upigaji penalti kutokana na kukosa penalti muhimu mbili kwenye michezo tofauti hivi karibuni.