Vini Jr amtabiria makubwa Lamine Yamal
Muktasari:
- Winga huyo wa Madrid alikuwa wazi na mwenye msisitizo alipoulizwa kuhusu nyota huyo wa Barça kwenye Caze TV.
MADRID, HISPANIA: Vinícius Júnior alizungumza katika mahojiano nchini Brazil kuhusu Lamine Yamal, akimsifu kwa kiwango chake kikubwa cha soka licha ya kuchezea FC Barcelona, wapinzani wakubwa wa milele wa Real Madrid CF.
Winga huyo wa Madrid alikuwa wazi na mwenye msisitizo alipoulizwa kuhusu nyota huyo wa Barça kwenye Caze TV.
“Hispania wana Lamine Yamal, ambaye ni mmoja wa wachezaji bora duniani. Anafanya mambo ya ajabu uwanjani. Ni mchezaji ambaye anaweza kushinda Kombe la Dunia. Ni mmoja wa wale wachezaji ambao watu hulipia kwenda kuwaangalia,” amesema.
“Kuongelea wachezaji wa Barcelona huwa ni jambo gumu kwa sababu mashabiki huanza kuzungumza, lakini tunapaswa kuthamini wachezaji waliopo uwanjani,” ameeleza Vini Jr.