Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Vigogo Newcastle United wanaogopa

VIGOGO Pict

Muktasari:

  • Liverpool, ambao ni mabingwa wa Ligi Kuu England msimu uliopita, wameonyesha wako tayari kusitisha kwa muda nia ya kumsajili Isak baada ya ofa yao ya Pauni 110 milioni kukataliwa na Newcastle.

NEWCASTLE, ENGLAND: MABOSI wa Newcastle wana hofu kwamba Liverpool iko tayari kutumia mbinu ya kusubiri kama ile ilivyofanya kwa Virgil van Dijk  ili kuhakikisha inainasa saini ya mshambuliaji Alexander Isak, ambaye thamani yake inakadiriwa kufikia Pauni 150 milioni.

Liverpool, ambao ni mabingwa wa Ligi Kuu England msimu uliopita, wameonyesha wako tayari kusitisha kwa muda nia ya kumsajili Isak baada ya ofa yao ya Pauni 110 milioni kukataliwa na Newcastle.

Isak, raia wa Sweden mwenye umri wa miaka 25, ametangaza nia ya kujiunga na Liverpool na kwa sasa anafanya mazoezi katika miundombinu ya klabu yake ya zamani, Real Sociedad, wakati wachezaji wenzake wa Newcastle wakiwa kwenye ziara ya maandalizi ya msimu mpya barani Asia, safari ambayo hakushiriki kutokana na majeraha madogo ya paja.

Hali hiyo imeanza kumweka pabaya mbele ya mashabiki wa Newcastle licha ya kocha Eddie Howe kusisitiza kuwa mchezaji huyo bado ni mchezaji wa timu na anapata msaada kamili klabuni.