Hello

Your subscription is almost coming to an end. Don’t miss out on the great content on Nation.Africa

Ready to continue your informative journey with us?

Hello

Your premium access has ended, but the best of Nation.Africa is still within reach. Renew now to unlock exclusive stories and in-depth features.

Reclaim your full access. Click below to renew.

Neville: Huyu Carrick anampa somo Amorim

Muktasari:

  • Kocha huyo wa mpito wa Man United aliimarisha matumaini ya klabu kumaliza ndani ya nafasi nne za juu kwa ushindi mwingine Jumatatu usiku, baada ya Mashetani Wekundu kuifunga Everton bao 1-0.

MANCHESTER, ENGLAND: GARY Neville anaamini kuwa kufufuka kwa Manchester United chini ya Michael Carrick kutamlazimisha Ruben Amorim kufanya mabadiliko atakaporejea tena kwenye ukocha.

Kocha huyo wa mpito wa Man United aliimarisha matumaini ya klabu kumaliza ndani ya nafasi nne za juu kwa ushindi mwingine Jumatatu usiku, baada ya Mashetani Wekundu kuifunga Everton bao 1-0.

Amorim, mwenye umri wa miaka 41, alifutwa kazi na Man United mwezi uliopita kufuatia sare ya 1-1 dhidi ya Leeds United na mfululizo wa ushindi mmoja tu katika mechi tano. Nafasi yake ilichukuliwa kwa muda na Darren Fletcher kwa safari ya Ligi Kuu dhidi ya Burnley na mchezo wa Kombe la FA nyumbani dhidi ya Brighton kabla Carrick hajateuliwa rasmi kuwa kocha mkuu hadi mwisho wa msimu.

Tangu arejee Old Trafford, Carrick, 44 ameonyesha athari kubwa, akiiongoza Man United kushinda mechi tano na kutoka sare moja katika michezo sita ya kwanza. Man United ilishinda mechi nne mfululizo dhidi ya Manchester City, Arsenal, Fulham na Tottenham Hotspur kabla ya sare ya 1-1 dhidi ya West Ham United kuvunja rekodi hiyo mapema mwezi huu.

Hata hivyo, Man United ilirejea kwenye ushindi kwa kuifunga Everton 1-0 katika Uwanja wa Hill Dickinson Jumatatu usiku. Matokeo hayo yameipandisha timu hiyo hadi nafasi ya nne, pointi tatu tu nyuma ya Aston Villa walio nafasi ya tatu, na kuwaweka kwenye nafasi nzuri ya kufuzu Ligi ya Mabingwa Ulaya.

Baada ya kuteuliwa kwake, Carrick aliachana na mfumo wa Amorim wa 3-4-2-1 na kuanzisha mfumo rahisi zaidi wa 4-2-3-1, na pia akamrejesha Kobbie Mainoo kikosini baada ya kutotumika chini ya kocha wa zamani. Carrick pia amefanya mabadiliko mengine kadhaa, ikiwamo kufupisha muda wa mazoezi ili yawe makali zaidi na kusogeza mbele kwa dakika 15 muda wa wachezaji kufika kambini kwa mechi za nyumbani na ugenini.

Huu ni mpango ambao umezaa matunda hadi sasa, na beki wa zamani wa Man United, Neville, anaamini mafanikio ya Carrick yatamlazimisha Amorim kubadili mbinu zake atakapopata kazi nyingine ya ukocha, aliposema: “Ni wazi alipata mambo kadhaa vibaya ukiangalia kinachoendelea sasa. Alibadilisha mfumo kidogo katika baadhi ya mechi na ikaonekana kama hiyo ingeweza kuwa njia sahihi. Lakini, dhidi ya Wolves alirudi kwenye mfumo ule ule na hiyo, kwangu mimi, ilikuwa kama pigo la mwisho kwa Ruben Amorim.

“Kisha ukiangalia kilichotokea kwa Mainoo, unamuona akicheza pamoja na Casemiro na wanaonekana kuwa jozi imara sana. Mainoo anaonekana kama mchezaji kamili wa mpira. Anaweza kucheza nafasi yake vizuri, ana uwezo wa kumiliki mpira, na anaonekana amerudi kwenye kiwango chake bora. Hilo linaonekana wazi..”

Katika kipindi chake cha miezi 14 akiwa kocha wa Man United, Amorim alishinda mechi 24 tu kati ya 63 katika mashindano yote.